TAARIFA HUKUJUZA MENGI YA ULIMWENGUNI

Jumatatu, 2 Mei 2016

SERIKALI YA MAGUFULI IMEPUNGUZA KODI KUTOKA ASILIMIA 11 HADI 9

Hakuna maoni
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe John Pombe Magufuli amesema serikali yake imepunguza makato ya kodi katika mishahara kutoka asilimia 11 mpaka 9 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa kwa kada hiyo huku akiahidi fedha zinazokusanywa katika vita ya ufisadi, ukwepaji kodi na watumishi hewa zitapelekwa kwenye miradi ya maendeleo na kuboresha maslahi
ya wafanyakazi ili kuongeza tija na ufanisi makazini.
Rais John Magufuli anatoa kauli hiyo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ambayo kitaifa yamefanyika mjini dodoma  ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu kuapishwa kuwa Rais ambapo anasema hatua hiyo itsaidia kupunguza ukali wa maisha hasa kwa wafanyakazi wa kawaida huku pia akitoa wito wa kufanya kazi kwa bidii.
 
Huku akishangiliwa na umati wa watu katika risala yake Rais Magufuli akatoa takwimu mpya za vita dhidi ya wafanyakazi hewa ambapo amesema hivi sasa wamefikia zaidi ya elfu kumi na bado mapambano yanaendelea.
 
Katibu mkuu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA Nicholaus Mgaya amesema bado sekta ya ajira nchini inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ongezeko la wageni kupora kazi za wazawa huku Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, vijana ajira na walemavu, Mh.Jenista Mhagama akibainisha kuwa serikali iko katika mkakati wa kuboresha maslahi ya wafanyakazi kulingana na viwango vilivyowekwa na shirika la kazi duniani (ILO).
 
Nao baadhi ya washiriki wa maadhimisho hayo wamepongeza kasi ya utendaji wa serikali ya awamu ya tano wakidai kuwa itakuwa chachu ya maendeleo kwa taifa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni