Rais wa Ufaransa amemtaka Rais mpya wa
Marekani aheshimu makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1
yaliyosainiwa huko Vienna nchini Austria Julai mwaka 2015.
Katika mazungumzo ya simu hapo jana, Rais Francois Hollande wa
Ufansa amemtaka mwenzake wa Marekani Donald Trump kuheshimu makubaliano
ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji
(JCPOA) baina ya Iran na madola sita makubwa duniani ambayo ni Marekani,
China, Russia, Ufaransa, Uingereza na Ujerumani.
Hollande amemtaka Trump azingatie taathira za baadaye za kisiasa na
kiuchumu iwapo ataamua kuchukua hatua zozote za kukiuka makubaliano hayo
ambayo yalianza kutekelezwa Januari mwaka jana. Rais Francois Hollande wa UfaransaMwezi uliopita, Rais Hassan Rouhani alisisitiza kuwa Iran
haitairuhusu Marekani ikiuke au iichane hati ya makubaliano ya nyuklia
ya (JCPOA).
Ikumbukwe kuwa, wakati wa kampeni za uchaguzi, Trump alitishia
kuyachana makubaliano ya nyuklia na Iran wakati atakapoingia katika
ikulu ya Marekani, White House. Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran alijibu msimamo huo wa Trump kwa kusema, makubaliano ya
nyuklia ya JCPOA ni azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na
hayawezi kuvunjwa kwa uamuzi wa serikali ya nchi moja.
Trump akisaini amri dhidi ya wakimbizi na wahamiajiWakati huo huo, Rais Francois Hollande wa Ufaransa amemtaka Trump
aheshimu kadhia ya kuwakubali wakimbizi nchini humo, na kuongeza kuwa,
azimio kuhusu mgogoro wa Syria linaweza kutekelezwa tu katika fremu ya
Umoja wa Mataifa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni