Katika semina hiyo iliyofanyika Dar es Salaam juzi, Balozi wa China nchini, Dk Lu Youqing alisema, nchi yake ina imani kubwa na Tanzania katika suala zima la kukua kwa viwanda kutokana na rasilimali nzuri na mazingira yake kuwezesha ustawi wa viwanda.
Alisema, katika nchi yoyote viwanda ndio vina nafasi ya pekee ya kubadilisha uchumi na kuleta maendeleo kwa haraka. Alisema, kwa sasa China ni miongoni mwa nchi zenye uchumi imara kutokana na kuwa na viwanda vingi.
“Kupitia sekta ya viwanda, tunaweza kuboresha na kuimarisha kilimo chetu, uchumi wetu na kujiletea maendeleo. China inazitia moyo nchi za Afrika kupata maendeleo kupitia viwanda,” alisema.
Alisema, Tanzania inahitaji kuwa ya viwanda ingawa kuna changamoto zinazoikabili, hivyo kuhitaji kutatuliwa. Aliongeza kuwa, asilimia 90 ya nchi za Afrika zimeshajua umuhimu wa viwanda, lakini baadhi hazina uwezo wala rasilimali za kuwezesha viwanda hivyo kufanya kazi.
Wakati huo huo, Dk Meru alisema, serikali itahakikisha sekta ya viwanda inatoa asilimia 40 ya ajira nchini ifikapo mwaka 2020 na kuchangia pato la taifa kwa asilimia 15, ifikapo mwaka huo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni