Wakizungumza katika mazishi hayo ,wamesema kutokana na kuwepo kwa
matukio ya radi kila mwaka, ni vyema Serikali ikasaidia kuweka kinga ili
kuokoa maisha ya wananchi ambao wamekuwa wakipoteza maisha kila mwaka
kutokana na kupigwa na radi na kwamba tukio hilo limeleta hofu kijijini
hapo.
Akizungumza baada ya kuongoza mazishi hayo kwa niaba ya Serikali ,
Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Bi.Ruth Msafiri amewataka wakazi wa kijiji
hicho kutohusisha tukio hilo na imani za kishirikina na kwamba serikali
itaangalia uwezekano wa kusaidiana na wananchi kuweka kinga ya kitaalam
katika Taasisi za Umma zenye mikusanyiko kama shule na Zahanati.
Katika tukio hilo wanafunzi wanne walikufa baada ya kupigwa na radi
wakiwa darasani na wengine tisa kujeruhiwa katika shule ya msingi
Nyaruyoba.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni