Polisi nchini Ujerumani wanawachunguza mume na mke ambao wanadaiwa kumfungia mwanao wa kiume ndani ya nyumba kwa miaka 30, katika jimbo la Bavaria
Mwanamme huyo wa miaka 43 hajawahi kuonekana hadharani tangu kuacha shule akiwa na miaka 13. Polisi wamesema japo mwanamme huyo yuko shwari kiafya, hata hivyo ameonekana kuwa na mfadhaiko.
Hata hivyo wamesema hawatawasilisha mashtaka yeyote. Polisi walijulishwa kuhusu tukio hilo na jirani ya mtu huyo ambapo walimchukua kutoka nyumba alikoishi na kumpeleka hospitalini.
Hata hivyo walikabiliwa na wakati mgumu kumshawishi bwana yule kupelekwa hospitailini. Mamake amesema mwanawe huyo hakufungiwa na kwamba ni yeye binafsi aliyekataa kwenda shule na kuamua kusalia ndani ya nyumba kwa miaka 30.
Maafisa wa hospitali alikolazwa wanajaribu kumfanyia uchunguzi wa kiakili. Wengi wanahoji kuhusu jinsi mtu huyo aliepuka ushawishi wa mitandao, ujana, huduma za kijamii na zile za kiafya bila kujulikana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni