TAARIFA HUKUJUZA MENGI YA ULIMWENGUNI

Jumamosi, 26 Machi 2016

Ng'ombe 1,294 wakamtwa ndani ya msitu wa Buhindi

Maoni 1


Jumla ya Ng’ombe 1,294 wamekamatwa ndani ya msitu wa taifa wa Buhindi,uliopo katika Halmashauri ya wilaya ya Buchosa Mkoani Mwanza,huku Wafugaji kumi na saba wanaomiliki Mifugo hiyo wakitozwa faini ya zaidi ya shilingi Milioni 200 katika zoezi la kuondoa Mifugo iliyomo ndani ya msitu huo.
Zoezi hilo la kuondoa Mifugo hiyo ndani ya Shamba la Misitu Buhindi limefanyika Jumapili iliyopita Machi 20,huku baadhi ya Wafugaji wakieleza kutoridhishwa na namna zoezi hilo lilivyotekelezwa kikiwemo kiwango kikubwa cha faini.
Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa,ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nyanzenda Bw.Idama Kibanzi amemlalamikia Meneja wa Msitu wa Buhindi Mohammed Hamis kwa kushindwa kutumia busara wakati wa ukamataji wa Mifugo hiyo na kusababisha mgogoro kati ya wafugaji na uongozi wa msitu huo.
Kaimu Katibu tawala wa wilaya ya Sengerema Aron Loshie Laizer amefika katika msitu huo wa Taifa wa buhindi ili kujionea uharibifu unaodaiwa kufanywa na Mifugo hiyo.
Msitu wa Buhindi uliandikishwa rasmi kisheria kuwa msitu wa hifadhi wa taifa mwaka 1995,katika tangazo la Serikali namba 346 na una jumla ya eneo la hekta 33,880 ambapo wanajamii wapatao 600 hujipatia ajira kila mwaka kwenye Viwanda vya kuchakata Magogo na kupakia mbao huku watu 200 wakifanya shughuli mbalimbali za ujasiriamali.

Maoni 1 :